KILIMO BORA CHA ZAO LA NYANYA


MUONGOZO WA KILIMO BORA CHA ZAO LA NYANYA KWA MAVUNO FURAHISHI
Image result for best harvest tomato
MPANGILIO WA MBOLEA NA VIUATILIFU KATIKA ZAO LA NYANYA SHAMBANI

·         KUANDAA SHAMBA.
Tumia sumu ya max round au max round turbo kuuwa viotelea na majani yote kabla ya kulima au kupanda nyanya shambani.

·         BAADA YA KUPANDIKIZA MICHE
Pulizia sumu ya wilstop siku 2-3 baada ya kupandikiza miche kuepusha uotaji wa magugu na viotelea aina zote shambani


·         WIKI YA 1-2 BAADA YA KUPANDIKIZA
Mbolea: weka mbolea ya DAP, Yara mila winner, au Yaramila otesha 50 kg kwa ekari kuchochea ukuaji wa mizizi na ustawi wa zao shambani.

Kudhibiti magonjwa ya ukungu/barafu: pulizia sumu ya super will, wilthane au wilzeb kukinga au kutibu magonjwa yote ya ukungu/kuvu shambani kama vile kata kiuno, bakajani wahi, bakajani chelewa, ubwiru chini, ubwiru unga.
Kumbuka: pulizia madawa ya ukungu kila baada ya wiki 1-2 kuepusha ueneaji wa magonjwa shambani.

Kudhibiti wadudu waharibifu: pulizia sumu ya dudumectin, wilcron au duduwill na wiltigo plus kudhibiti jamii yote ya wadudu waharibifu, kama vile KANITANGAZE, vipepeo weupe, leaf minner, vimamba n.k

·         WIKI YA 3-4 BAADA YA KUPANDIKIZA
Mbolea: weka mbolea ya kukuuzia kama vile NPK, Yara mila winner, UREA, n.k 50 kg/ekari ili kustawisha mmea Zaidi shambani.
Kumbuka kupiga dawa ya ukungu kila baaada ya wiki 1-2 na kupiga dawa ya wadudu waharibifu shambani kwa afya nzuri ya mmea.

·         MAUWA YAKIANZA KUSHAMIRI
Mbolea; weka mbolea ya yaraliva nitrabor au yaraliva calcinity 50 kg/ekari
Pulizia sumu ya wiltigo plus changanya na sumu ya wilcron, dudumectin au duduwill kudhibiti KANITANGAZE na wadudu wengine wote waharibifu.
·         MATUNDA YAKISHA TOKA
Mbolea: weka mbolea ya yaraliva nitrabor chanaganya na NPK/ yaramila winner/CAN/ UREA kujenga nyanya yenye Afya, umbo kubwa na kuongeza maisha rufani baada ya kuvunwa.
Pulizia super will kukinga dhidi ya magonjwa ya kuvu kama vile ubwiru chini, ubwiru unga

SOMA: MUONGOZO MFUPI KILIMO CHA TIKITI MAJI

MAWASILIANO: 0757 139 423 Mr Mpinga, mtaalamu na mshauri wa kilimo

MAKALA HII NI KWA MUJIBU WA AGRONOMIST WA SEMINIS NA BIDDI ENTEPRISES LTD. Mr. Mpinga

Maoni

Chapisha Maoni

Machapisho Maarufu