FAHAMU NAMNA NA FAIDA YA KUPUNGUZA MATAWI YA MATIKITI MAJI.

FAHAMU NAMNA, FAIDA NA HASARA YA KUPUNGUZIA MATAWI YA MATIKITI MAJI.


Imeandaliwa na Mr Mpinga Agronomist CONTINENTAL SEEDS COMPANY. 
+255 757 139 423.
kilimoforlife@gmail.com 
Instargram: kilimo for life.

BONYEZA HAPA KUPATA FOMULA ZA KILIMO


Habari Mpendwa msomaji wa makàla zetu za kilimo cha mazao mbalimbali kupitia
mtandao wetu wa Kilimo for life: Kilimo for life ni blog ya kilimo inayosomwa zaidi nchini kwa sasa.

Leo nitaelezea juu ya faida, Namna na hasara ya upunguziaji wa matawi katika shina la Tikiti maji.

Kwasababu mashina ya tikiti maji yanatabia ya kutambaa umbali wa mita 2 na zaidi, huwenda kuna haja ya kupunguza matawi ??

JE KUNA FAIDA YA KUPUNGUZA MATAWI YA MATIKITI MAJI. 

FAIDA
Punguza matawi yanayozidi umbali wa nafasi zilizoandaliwa ili kuepusha mbanano baina ya mashina ya tikiti maji.

Kupunguza matawi ya tikiti maji, inasaidia kuelekeza virutubisho kwenye matawi mengine hivyo kufanya matawi mengine kuwa manene, yenye Afya.

Endapo matawi mengine yatakuwa na afya tutaraji matunda kuwa na afya na saizi kubwa zaidi.

NAMNA YA KUPUNGUZIA MATAWI
Tumia mkasi safi au prunner kukata tawi bovu au lisilo na mauwa mengi au matunda. Kata karibu na pale linapounganikia na tawi kuu.

Kata matawi yasiyo na afya nzuri, matawi yenye ugonjwa, matawi yenye umanjano, matunda mabovu, matunda yenye umbo baya n.k

JE KUNA HASARA YA KUPUNGUZIA MATAWI???

JIBU
Huenda katika kupunguza matawi kukasababaisha kupoteza mauwa jike ambayo huwa ni machache kuliko mauwa dume.
Uwa jike

Huenda katika kupunguza matawi kukasababisha kueneza magonjwa kupitia majeraha 

Kupunguzia matawi kunasabibisha kuongezeka magugu ambayo huzuiwa na matawi mengi ya Tikiti maji.



CHAKUZINGATIA
Punguzia matawi kipindi kikavu: Namaanisha epuka kupunguzia matawi kipindi cha unyevu nyevu mwingi, mvuwa au mtuamo wa maji ili kuepuka magonjwa mbalimbali ambayo huenea zaidi kipindi cha unyevu na mvuwa au mtuamo wa maji.

MWISHO.

WASILIANA NASI KWA MSAADA NA USHAURI KUHUSIANA NA KILIMO CHA MAZAO YOTE. 

MENGU ZOTE ZINAPATIKANA +255 757 139 423.

ARUSHA TANZANIA.


COMMANDO F1.

SUPER BELL F1 

Maoni

  1. Nimeioana makala yako, iko vizuri endelea kuweka nyingine mtandaoni

    JibuFuta

Chapisha Maoni

Machapisho Maarufu