MBEGU BORA ZAIDI ZA TIKITI MAJI TANZANIA

MBEGU BORA ZA TIKITI MAJI TANZANIA




Na Abbas Mpinga

Habari Mpendwa msomaji wa makàla zetu za kilimo cha mazao mbalimbali kupitia mtandao wetu wa Kilimo for life
Kilimo for life inakusudia kuhamasisha na kufundisha wakulima kuwekeza kwenye kilimo biashara kwa kulima kitaalamu zaidi kwa kuzingatia uchaguzi sahihi wa mbegu bora kulingana na ukanda pia matumizi sahihi ya mbolea na viuatilifu kwa wakati sahihi na zaidi ni kufuata kanuni bora za Agronomia kwa matunzo ya mazao shambani.

Kama tulivyokwisha ainisha juu ya mambo ya kuzingatia katika kilimo bora chenye faida cha zao la tikiti maji, leo tutaorodhesha mbegu bora zaidi za tikiti maji zinazopatikana Tanzania.

Lengo ni kusaidia wakulima wetu wafahamu mbegu bora kulingana na soko lililopo  ili waweze kunufaika na kilimo chao.

1. ANITA F1

Hii ni mbegu inayofanya vizuri zaidi nyakati zote kwa kanda zote

Ina rangi ya zebra kwa juu

Inastahimili Hali zote za mazingira (JOTO na BARIDI)

Inazaa kwa haraka zaidi siku 75

Inazaa tunda la uzito wa Kilo 8 hadi 12

2 SHABIKI F1
Hii ni mbegu inayofanya vizuri zaidi nyakati zote kwa kanda zote

Ina rangi ya zebra kwa juu


Asili yake ni kenya

Inastahimili Hali zote za mazingira (JOTO na BARIDI)

Inazaa kwa  siku 80

Inazaa tunda la uzito wa Kilo 8 hadi 15


3.SUKARI F1 F1 F1

Hii ni mbegu inayofanya vizuri kwa kanda zote (JOTO na BARIDI)

Ina Rangi ya zebra kwa juu

Tunda lake Lina shape ya duara Butu (duara iliyorefuka)

Inazaa kwa muda wa siku 75 hadi 80

Inazaa Tunda la uzito wa Kilo 8 hadi 12

4. ASALI F1

 Hii ni mbegu inayofanya vizuri kwa kanda zote (JOTO na BARIDI)

Ina Rangi ya zebra Mpauko kwa juu

Umbo la Tunda ni duara

Tunda lake ni tamu sana

Inazaa kwa muda wa siku 80

Inazaa Tunda la uzito wa Kilo 8 hadi 15

PATO F1 


Hii ni mbegu nzuri kwa kanda zote

Ina Rangi ya zebra kwa juu

Inazaa kwa muda wa siku 80 hadi 85

Inazaa Tunda la uzito wa Kilo 8 hadi 10

KUMBUKA: Mbegu zote ni Bora na  zimethibitishwa na Ofisi ya Taasisi ya kuthibitisha ubora wa mbegu Tanzania (TOSCI).

PIA, kuna Aina nyingi zaidi za mbegu za tikiti ambazo hatujaziorodhesha hapo juu; Hili tumezingatia mbegu bora na shindani kulingana na uhitaji Sokoni

Mbegu zingine ni 

Zebra F1
Sugarking F1
Sugar queen F1
Mkombozi F1
Apoorva F1 


ZAIDI
KWA USHAURI NA MAHITAJI YA MBEGU NA BIDHAA ZOTE ZA KILIMO
WASILIANA NA KILIMO FOR LIFE KWA MSAADA ZAIDI

Simu:  +255 757 139 423

Au
Baruwa pepe: Kilimoforlife@gmail.com

INSTAGRAM- Kilimo for life

FACEBOOK: Kilimo for life au Abbas Mpinga

Maoni

  1. Enter your comment...
    Asante sana kiongozi. tunaomba tuone uwezo wakutoa matunda kwa kila aina ya mbegu apo juu. kwa mkulima Mavuno ndo key performance indicator.
    Nashukuru

    JibuFuta
  2. Vizuri sana mtalaam kwa somo fupi na nzuri.

    JibuFuta
  3. Elimi nzuri sana hongereni kwa maono makubwa
    Lakini mbona tunajiunga kwenye kundi la whatsap halikubali? Lakini pia mko sehemu gani ya Tanzania? Vp kuhusu bei ya hizo mbegu? Pia ni mbegu gani ambayo ni mpya zaidi sokoni ukilinganisha na Hali ya hewa ya sasa?

    JibuFuta

Chapisha Maoni

Machapisho Maarufu