FAHAMU GHARAMA KATIKA KILIMO CHA NYANYA


MPANGILIO HAFIFU WA GHARAMA KATIKA KILIMO CHA NYANYA TANZANIA
Image result for tomato crop

Na Mr. MPINGA

Hapa nitaelezea, kujulisha, kuainisha, na kudadavuwa juu ya gharama za kilimo cha nyanya kwa uchache Zaidi.
kulingana na utofauti wa kikanda na mazingira, nitajulisha gharama za manejimenti ya shamba pekee; yaani gharama za mbegu, madawa na mbolea zinazohitajika kwenye shamba la nyanya kuanzia mwanzo hadi mavuno.
Gharama za kodi ya shamba, umwagiliaji, wafanyakazi na miundombinu ya shambani haitoainishwa kulingana na kutofautiana kwa gharama hizi kulingana na eneo au ukanda husika.
NUNUA FORMULA YA KILIMO CHA NYANYA KWA MPANGILIO SAHIHI WA MBOLEA NA VIUATILIFU 


Gharama hizi zitakuwa kwa eneo la ekari moja pekee
Hii itasaidia mkulima kufahamu, kujuwa na kupanga bajeti ya ujumla kabla ya kuanza mradi wa kilimo cha nyanya.

Ikumbukwe kuwa; zao la nyanya shambani ni Zaidi ya mtoto mchanga katika malezi na matunzo; zao la nyanya linahitaji umakini mkubwa sana katika kipindi chote cha ukuwaji mpaka hadi mavuno. Maana hii ni kwamba; Smkulima anapaswa kutembelea na kujuwa hali na maendeleo ya ukuwaji wa shamba kila siku.


MABEGU BORA ZA NYANYA NA GHARAMA ZAKE
JINA LA MBEGU
KIASI KWA EKARI
BEI YA MBEGU

AINA
MSIMU/HALI YA HEWA

COMMANDO F1
30-40 gm
240000
MSHUMAA
BARIDI/MVUWA NYINGI
SIFA F1
30 gm
330000
MSHUMAA
JOTO/ MVUWA CHACHE
RANGER F1 
30 gm
330000
MSHUMAA
JOTO,MNYAUKO, BARIDI, MVUWA NYINGI
SIFA F1
30 gm

MSHUMAA
MAZINGIRA YOTE




MADAWA YA UKUNGU NA GHARAMA ZAKE KWA EKARI MOJWA
madawa ya kudhibiti magonjwa ya fangasi/ukungu/barafu/kuvu hupaswa kupigwa mara zaidi shambani kuliko madawa ya wadudu.

mkulima anapaswa kupiga madawa ya fangasi kila baada ya siku 7 hadi 14, kulinagana na ahali aya hewa.

kwa kipindi cha mvuwa nyingi; mkulima atapaswa kupiga dawa kila baada ya siku 7.
 ni vyema kupiga dawa ya kukinga au kutibu na kukinga kabla ugonjwa haujaonekana au kutokea.

kwa mantiki hiyo ni kwamba waweza tumia dawa yeyote kati ya hizi zilizoorodheshwa chini kwa kukinga.

na kama ugonjwa umekwisha ingia; itabidi upige dawa ya kukinga na kutibu.


GHARAMA ZA MADAWA YA WADUDU.

Wadudu wasumbufu Zaidi kwenye zao la nyanya namba moja ni KANITANGAZE, ikifuatiwa na vipepeo weupe, vimamba, leaf miners n.k
Wadudu hawa hudhibitiwa vizuri Zaidi kwa kupiga dawa mchanganyiko wa dudumectin au wilcron na wiltigo plus.
Wiltigo plus inauwezo mkubwa Zaidi wa kumdhibiti kanitangaze kwani hutoa kinga ya muda mrefu Zaidi (siku 21).
Hivyo ninawashauri wakulima kutumia Amsac, Liberity, belt, Couragen kuanzia mara tu utakapopandikiza miche shambani mpaka hadi mavuno.


Changanya kiasi cha 5 mls wiltigo plus na 30 mls dudumectin au wilcron katika lita 16 hadi 20 za maji.
Kumbuka kupiga dawa ya wiltigo plus kila baada ya siku 14-21 ili kuweka kinga dhidi ya kanitangaze,mdudu hatari Zaidi kwa zao la nyanya.


GHARAMA ZA MBOLEA KATIKA ZAO LA NYANYA.
MUDA BAADA YA KUPANDIKIZA
MBOLEA
KIASI KWA EKARI
GHARAMA
WIKI 1-2
DAP (bora)
50 Kg
66,000- 67,000
YARAMILA OTESHA (bora Zaidi)
50 Kg
63,000-65,000
YARAMILA WINNER
50 Kg
65,000 – 68,000
WIKI 3-4
YARAMILA WINNER (bora Zaidi)
50 Kg
65,000 – 68,000
YARAVERA AMIDAS
50 kg
57,000 -58,000
UREA
50 Kg
56,000
NPK (bora)
50 Kg
59,000-61,000/=
MAUWA YA KIKARIBIA KUTOKA
YARALIVA NITRABOR (bora Zaidi)
50 kg
70,000-74,000/=
CAN
50 kg
43,000-45,000/=
MATUNDA YAKITOKA
YARALIVA NITRABOR+ NPK/ WINNER
25 Kg : 50 kg
35,000 + 59,000/68,000/=
BAADA YA MCHUMO WA KWANZA
YARALIVA NITRABOR+ NPK/ WINNER
25 Kg : 50 kg
35,000 + 59,000/68,000/=

MAELEZO: katika orodha tajwa ya mbolea hapo juu, mbolea zote ni bora Zaidi kutumika nimezipaka kwa rangi ya njano.
NB: mbolea ya samadi haijainishwa kutokana na utofauti wa gharama kulingana na eneo.
Ni bora Zaidi kutumia mbolea ya samadi kabla ya kupandikiza miche shambani.
Hivyo kwa Makala hii gharzima mkulima ataamuwa atumie mbegu ipi, dawa zipi, na mbolea zipi kwa ghaarama ipi ili kufanikisha mradi mzima wa kilimo cha nyanya.

Shukrani sana kwa kusoma Makala zangu.

KWA USHAURI NA MAHITAJI YA MBEGU, MBOLEA N.K WASILIANA NAMI


WASILIANA NAMI KWA 0757 139 423 Mr Mpinga Agronomist na mshauri wa masuala ya kilimo

kilimoforlife@gmail.com

Maoni

  1. Hongera mtaalam, umetoa mfafanuzi mzuri

    JibuFuta
  2. Maoni haya yameondolewa na mwandishi.

    JibuFuta
  3. Nashukuru kwa masomo yenu. Je naweza kutumiwa watsap?
    Namba yangu,0687987724

    JibuFuta
  4. Ahsante sana..vipi nyanya au mbengu nzuri ya kulima kwenye mkoa wenye mvua nyingi kama Kagera

    JibuFuta

Chapisha Maoni

Machapisho Maarufu